Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Shemu
Mwanzo 5 : 32
32 Baada ya Nuhu kufikisha umri wa miaka mia tano, aliwazaa Shemu, na Hamu, na Yafethi.
Mwanzo 6 : 10
10 Nuhu akazaa wana watatu wa kiume, Shemu, na Hamu, na Yafethi.
Mwanzo 7 : 13
13 Siku ile ile Nuhu akaingia katika safina, yeye, na Shemu na Hamu na Yafethi, wana wa Nuhu, na mkewe Nuhu, na wake watatu wa wanawe pamoja naye;
Mwanzo 9 : 18
18 Wana wa Nuhu waliotoka katika safina, ni Shemu, na Hamu, na Yafethi; na Hamu ndiye baba wa Kanaani.
1 Mambo ya Nyakati 1 : 4
4 na Nuhu, na Shemu, na Hamu, na Yafethi.
Mwanzo 9 : 27
27 ⑥ Mungu amwongezee Yafethi. Na akae katika hema za Shemu; Na Kanaani awe mtumwa wake.
Mwanzo 10 : 1
1 Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.
Mwanzo 10 : 31
31 Hao ndio wana wa Shemu, kufuata jamaa zao, na lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao.
Mwanzo 11 : 29
29 Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori aliitwa Milka, binti Harani, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska.
1 Mambo ya Nyakati 1 : 54
54 na jumbe Magdieli, na jumbe Iramu. Hao ndio majumbe wa Edomu.
Luka 3 : 36
36 ⑯ wa Kenani, wa Arfaksadi, wa Shemu, wa Nuhu, wa Lameki,
Leave a Reply