Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Shauri
Mithali 1 : 5
5 mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.
Mithali 9 : 9
9 ② Mwelimishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima; Mfundishe mwenye haki, naye atazidi kuwa na elimu;
Mithali 11 : 14
14 Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
Mithali 12 : 15
15 ② Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
Mithali 15 : 22
22 Pasipo ushauri mipango vuhunjika; Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.
Mithali 19 : 20
20 Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.
Mithali 20 : 18
18 Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.
Mithali 24 : 6
6 Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.
Mithali 1 : 33
33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya.
1 Wafalme 12 : 16
16 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli wakaenda zao hemani kwao.
Mathayo 19 : 22
22 Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Leave a Reply