Biblia inasema nini kuhusu Raha – Mistari yote ya Biblia kuhusu Raha

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Raha

Ayubu 20 : 16
16 Atanyonya sumu ya majoka; Na ulimi wa fira utamwua.

Ayubu 21 : 13
13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafla.

Mithali 9 : 17
17 ⑥ Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza.

Mithali 15 : 21
21 ② Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.

Mithali 21 : 17
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.

Mhubiri 1 : 17
17 Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kufukuza upepo.

Mhubiri 2 : 13
13 Ndipo nilipoona ya kuwa kweli hekima hupita upumbavu, kwa kadiri nuru ipitavyo giza;

Isaya 5 : 12
12 ⑱ Na kinubi, na zeze, na matari, na filimbi, na mvinyo, zote ziko katika karamu zao; lakini hawaiangalii kazi ya BWANA wala kuyafikiri matendo ya mikono yake.

Isaya 22 : 13
13 na kumbe! Furaha, na kuchekelea, na kuchinja ng’ombe, na kuchinja kondoo, na kula nyama, na kunywa mvinyo; tule, tunywe, kwa maana kesho tutakufa.

Isaya 47 : 9
9 ④ lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kamili, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno.

Amosi 6 : 1
1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na hao wanaokaa salama katika mlima wa Samaria, watu mashuhuri wa taifa lililo la kwanza, ambao nyumba ya Israeli huwaendea.

Luka 8 : 14
14 Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lolote.

Warumi 1 : 32
32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.

2 Wathesalonike 2 : 12
12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.

1 Timotheo 5 : 6
6 Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.

2 Timotheo 3 : 4
4 ⑪ wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;

Tito 3 : 3
3 Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.

Waraka kwa Waebrania 11 : 26
26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *