Biblia inasema nini kuhusu pumzi – Mistari yote ya Biblia kuhusu pumzi

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia pumzi

Ayubu 33 : 4
4 Roho ya Mungu imeniumba, Na pumzi za Mwenyezi hunipa uhai.

Mwanzo 2 : 7
7 BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa kiumbe hai.

2 Timotheo 3 : 16
16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

Ayubu 27 : 3
3 (Kwa kuwa uhai wangu ungali mzima ndani yangu, Na Roho ya Mungu iko katika pua yangu;)

Yohana 20 : 22
22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.

Ayubu 34 : 14 – 15
14 ⑯ Kama akimwekea mtu moyo wake, Akijikusanyia roho yake na pumzi zake;
15 Wenye mwili wote wangeangamia pamoja, Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.

Ezekieli 37 : 9
9 Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapulizie hawa waliouawa, wapate kuishi.

Isaya 42 : 5
5 ⑮ Mungu BWANA anena, yeye aliyeziumba mbingu, na kuzitanda; yeye aliyeitandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *