Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Pharez
Mwanzo 38 : 29
29 Ikawa aliporudisha mkono wake, tazama, ndugu yake akatoka. Akasema, Mbona umepita kwa nguvu wewe? Mambo ya nguvu na yakuandame. Kwa hiyo jina lake likaitwa Peresi[19]
1 Mambo ya Nyakati 2 : 4
4 ④ Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.
Mwanzo 46 : 12
12 Na wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela, na Peresi, na Zera; lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani. Na wana wa Peresi, ni Hesroni, na Hamuli.
Hesabu 26 : 21
21 Na wana wa Peresi walikuwa; wa Hesroni, jamaa ya Wahesroni; wa Hamuli, jamaa ya Wahamuli.
1 Mambo ya Nyakati 2 : 5
5 ⑤ Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.
1 Mambo ya Nyakati 9 : 4
4 Uthai, mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imli, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Nehemia 11 : 4
4 Tena wakakaa Yerusalemu wengine wa wana wa Yuda, na wengine wa wana wa Benyamini. Wa wana wa Yuda; Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, wa wana wa Peresi;
Nehemia 11 : 6
6 Wana wa Peresi wote waliokaa Yerusalemu walikuwa watu mia nne sitini na wanane, mashujaa.
Mathayo 1 : 3
3 Yuda akamzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu;
Luka 3 : 33
33 ⑭ wa Aminadabu, wa Admini, wa Hesroni, wa Peresi, wa Yuda,
Leave a Reply