Biblia inasema nini kuhusu Perizzites – Mistari yote ya Biblia kuhusu Perizzites

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Perizzites

Mwanzo 13 : 7
7 ⑤ Kukawako ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abramu, na wachunga wanyama wa Lutu; na siku zile Wakanaani na Waperizi walikuwa wakikaa katika nchi.

Mwanzo 15 : 20
20 na Mhiti, na Mperizi, na Mrefai,

Kutoka 3 : 8
8 ⑫ nami nimeshuka ili niwaokoe kutoka kwa mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hadi nchi njema, kisha pana; nchi itiririkayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.

Kutoka 23 : 23
23 ④ Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako, na kukufikisha kwa Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhivi, na Myebusi; nami nitawatupilia mbali.

Kumbukumbu la Torati 20 : 17
17 lakini uwaangamize kabisa, Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, kama alivyokuamuru BWANA, Mungu wako;

Waamuzi 3 : 7
7 Wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya BWANA, nao wakamsahau BWANA, Mungu wao, nao wakawatumikia Mabaali na Maashtorethi.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *