Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Nyuki
Kumbukumbu la Torati 1 : 44
44 ③ Na Waamori waliokuwa wakikaa katika mlima huo, waliwatokea juu yenu, wakawafukuza, kama wafukuzwao na nyuki, wakawapigia Seiri mpaka Horma.
Waamuzi 14 : 8
8 Kisha baadaye akarudi ili kumtwaa, naye akaenda kando kuuangalia mzoga wa huyo simba; na tazama, nyuki wengi walikuwamo ndani ya mzoga wa simba, na asali.
Zaburi 118 : 12
12 ⑫ Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la BWANA niliwakatilia mbali.
Isaya 7 : 18
18 Tena itakuwa katika siku hiyo BWANA atampigia kelele inzi aliye katika pande za mwisho za mito ya Misri, na nyuki aliye katika nchi ya Ashuru
Leave a Reply