Biblia inasema nini kuhusu Nyoka – Mistari yote ya Biblia kuhusu Nyoka

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Nyoka

Mwanzo 3 : 15
15 ⑱ nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.

2 Wakorintho 11 : 3
3 ⑪ Lakini nahofu; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

Mwanzo 3 : 1
1 ⑦ Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

Mhubiri 10 : 8
8 Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake; Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

Mathayo 10 : 16
16 Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwamwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.

Mwanzo 3 : 15
15 ⑱ nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.

Mwanzo 49 : 17
17 Dani atakuwa nyoka barabarani, Bafe katika njia, Aumaye visigino vya farasi, Na apandaye akaanguka chali.

Mwanzo 3 : 14
14 ⑰ BWANA Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;

Isaya 65 : 25
25 Mbwamwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema BWANA.

Mika 7 : 17
17 Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa BWANA, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako.

Mathayo 7 : 10
10 Au akiomba samaki, atampa nyoka?

Kumbukumbu la Torati 32 : 24
24 Watakonda kwa njaa, wataliwa na makaa ya moto, Na uharibifu mkali; Nitawapelekea meno ya wanyama wakali, Pamoja na sumu ya wadudu watambaao mavumbini.

Kumbukumbu la Torati 32 : 33
33 Mvinyo yao ni sumu ya majoka, Uchungu mkali wa nyoka.

Ayubu 20 : 16
16 Atanyonya sumu ya majoka; Na ulimi wa fira utamwua.

Zaburi 58 : 4
4 ④ Wana sumu mfano wa sumu ya nyoka; Wao ni kama fira kiziwi azibaye sikio lake.

Zaburi 140 : 3
3 Wamenoa ndimi zao na kuwa kama za nyoka, Na katika midomo yao mna sumu ya fira.

Mithali 23 : 32
32 Mwisho wake huuma kama nyoka; Huchoma kama fira.

Matendo 28 : 6
6 Wao wakadhani ya kuwa atavimba au kuanguka chini kwa kufa ghafla; na wakiisha kumwangalia sana, na kuona kwamba halimpati dhara lolote, wakageuka, wakasema kwamba yeye ni mungu.

Kutoka 4 : 3
3 Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia kutoka mbele yake.

Kutoka 7 : 15
15 Mwendee Farao asubuhi; tazama, atoka kwenda majini; nawe simama karibu na ufuo wa mto ili upate kuonana naye; na ile fimbo iliyogeuzwa kuwa nyoka utaichukua mkononi mwako.

Hesabu 21 : 7
7 Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa BWANA, atuondolee nyoka hawa. Basi Musa akawaombea watu.

Kumbukumbu la Torati 8 : 15
15 ⑰ aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu,

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *