Biblia inasema nini kuhusu Nondo – Mistari yote ya Biblia kuhusu Nondo

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Nondo

Ayubu 4 : 19
19 Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo, Ambazo misingi yao i katika mchanga, Hao wanaopondwa kama nondo!

Ayubu 27 : 18
18 Yeye hujenga nyumba yake kama mdudu, Na kama kibanda afanyacho mlinzi.

Zaburi 39 : 11
11 Ukimrudi mtu kwa kumkemea kwa uovu wake, Watowesha uzuri wake kama nondo. Kila mwanadamu ni ubatili.

Ayubu 13 : 28
28 Nijapokuwa ni kama kitu kilichooza, kinachosinyaa, Mfano wa nguo iliyoliwa na nondo.

Isaya 50 : 9
9 ⑤ Tazama, Bwana MUNGU atanisaidia; ni nani atakayenihukumu kuwa mwenye hatia? Tazama hao wote watachakaa kama vazi; nondo atawala.

Isaya 51 : 8
8 Maana nondo atawala kama vazi, na funza atawala kama sufu; bali haki yangu itakuwa ya milele, na wokovu wangu hata vizazi vyote.

Hosea 5 : 12
12 Kwa sababu hiyo mimi nimekuwa kama nondo kwa Efraimu, nimekuwa kama ubovu kwa nyumba ya Yuda.

Mathayo 6 : 20
20 bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wezi hawavunji wala hawaibi;

Yakobo 5 : 2
2 Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *