Biblia inasema nini kuhusu Ndege – Mistari yote ya Biblia kuhusu Ndege

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Ndege

Mwanzo 1 : 30
30 na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.

Mwanzo 1 : 26
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila kiumbe kitambaacho nchini.

Mwanzo 1 : 28
28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuimiliki; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Mwanzo 9 : 3
3 Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa mboga za majani, kadhalika nawapa hivi vyote.

Zaburi 8 : 8
8 Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini.

Yeremia 27 : 6
6 Na sasa nimetia nchi hizi zote katika mkono wa Nebukadneza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu; na wanyama pori pia nimempa wamtumikie.

Danieli 2 : 38
38 na kila mahali wakaapo wanadamu, wanyama wa kondeni na ndege wa angani amewatia mkononi mwako, naye amekumilikisha juu ya hao wote; wewe u kichwa kile cha dhahabu.

Yakobo 3 : 7
7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.

Mwanzo 9 : 3
3 Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa mboga za majani, kadhalika nawapa hivi vyote.

Kumbukumbu la Torati 14 : 20
20 Mna ruhusa kula katika ndege wote walio safi.

Mambo ya Walawi 11 : 20
20 Tena vyote vitambaavyo vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne, hivi ni machukizo kwenu.

Ayubu 38 : 41
41 ⑪ Ni nani anayempatia kunguru chakula, Makinda yake wanapomlilia Mungu, Na kutangatanga kwa kutindikiwa na chakula?

Zaburi 147 : 9
9 Humpa mnyama chakula chake, Wana-kunguru waliao.

Mathayo 10 : 29
29 Je! Mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu;

Luka 12 : 6
6 Je! Shomoro watano hawauzwi kwa senti mbili? Wala hasahauliwi hata mmojawapo mbele za Mungu.

Luka 12 : 24
24 ① Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, lakini Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!

Zaburi 104 : 12
12 Kandokando hukaa ndege wa angani; Na kuimba wakiwa katika matawi.

Mhubiri 12 : 4
4 ③ Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kushtuka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;

Wimbo ulio Bora 2 : 12
12 Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kuimba umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *