Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia ndege
Mathayo 6 : 26
26 ⑥ Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kuliko hao?
Kumbukumbu la Torati 22 : 6 – 7
6 ⑱ Kiota cha ndege kikitukia kuwa mbele yako njiani, katika mti wowote, au chini, chenye makinda au mayai, naye koo ameatamia juu ya makinda, au juu ya mayai, usimtwae yule koo pamoja na makinda;
7 ⑲ sharti umwache yule koo aende zake, lakini makinda waweza kuyatwaa uwe nayo; ili upate kufanikiwa, ufanye siku zako kuwa nyingi.
Ayubu 12 : 7 – 10
7 Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha; Na ndege wa angani, nao watakuambia;
8 Au nena na nchi, nayo itakufundisha; Nao samaki wa baharini watakutangazia.
9 Katika hawa wote ni yupi asiyejua, Kwamba ni mkono wa BWANA uliofanya haya?
10 Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake, Na pumzi zao wanadamu wote.
Leave a Reply