Biblia inasema nini kuhusu nafsi – Mistari yote ya Biblia kuhusu nafsi

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia nafsi

Ezekieli 18 : 4
4 Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu, ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu; roho ile itendayo dhambi itakufa.

Mathayo 10 : 28
28 ⑤ Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika Jehanamu.

Mhubiri 12 : 7
7 ⑤ Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.

Matendo 2 : 41
41 ⑲ Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapatao elfu tatu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *