Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mzee
Kumbukumbu la Torati 1 : 13
13 Jitwalieni watu wenye akili na fahamu, watu wanaojulikana, kwa kadiri ya makabila yenu, nami nitawafanya wawe vichwa juu yenu.
Matendo 11 : 30
30 Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.
Matendo 14 : 23
23 ⑫ Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.
Matendo 15 : 35
35 Na Paulo na Barnaba wakakaa huko Antiokia, wakifundisha na kulihubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.
Matendo 16 : 5
5 Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.
Matendo 20 : 17
17 Toka Mileto Paulo akatuma watu kwenda Efeso, akawaita wazee wa kanisa.
Matendo 20 : 32
32 Basi, sasa nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa.
Matendo 21 : 18
18 Hata kesho yake Paulo akaingia kwa Yakobo pamoja nasi, na wazee wote walikuwako.
1 Timotheo 4 : 14
14 ⑳ Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
1 Timotheo 5 : 19
19 Usikubali mashitaka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.
Tito 1 : 9
9 akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.
Waraka kwa Waebrania 11 : 2
2 Maana kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa.
Yakobo 5 : 15
15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
1 Petro 5 : 5
5 ⑯ Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.
2 Yohana 1 : 1
1 Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuayo ile kweli;
3 Yohana 1 : 1
1 Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli.
Ufunuo 4 : 4
4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti niliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wameikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji la dhahabu.
Ufunuo 4 : 10
10 ndipo hao wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi, nao humsujudia yeye aliye hai hata milele na milele, nao hutupa taji zao mbele ya kile kiti cha enzi, wakisema,
Ufunuo 5 : 5
5 Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila la Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na ile mihuri yake saba.
Leave a Reply