Biblia inasema nini kuhusu Mvua – Mistari yote ya Biblia kuhusu Mvua

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mvua

Mwanzo 7 : 4
4 ⑩ Kwa maana baada ya siku saba nitainyeshea dunia mvua, siku arubaini mchana na usiku; na kila kilicho hai nilichokifanya juu ya uso wa nchi nitakifutilia mbali.

Mwanzo 7 : 12
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arubaini mchana na usiku.

Mwanzo 7 : 24
24 ⑳ Maji yakapata nguvu juu ya nchi siku mia na hamsini.

Kutoka 9 : 26
26 Katika nchi ya Gosheni peke yake, walikokaa wana wa Israeli, haikuwako mvua ya mawe.

Kutoka 9 : 34
34 Farao alipoona ya kwamba mvua na mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akazidi kufanya dhambi, na kuufanya moyo wake mzito, yeye na watumishi wake.

1 Samweli 12 : 19
19 ③ Watu wote wakamwambia Samweli, Tuombee watumishi wako kwa BWANA, Mungu wako, tusije tukafa; maana tumeongeza dhambi zetu zote kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme.

1 Wafalme 18 : 45
45 Ikawa, muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini, akaenda zake Yezreeli.

2 Samweli 5 : 21
21 Nao wakaziacha sanamu zao huko, na Daudi na watu wake wakaziondolea mbali.

Isaya 28 : 21
21 ⑤ Maana BWANA ataondoka kama vile katika mlima Perasimu, ataghadhibika kama vile katika bonde la Gibeoni; apate kufanya kazi yake, kazi yake ya ajabu; na kulitimiza tendo lake, tendo lake la ajabu.

Mithali 25 : 23
23 Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu.

Kumbukumbu la Torati 11 : 17
17 hasira za BWANA zikawaka juu yenu, naye akafunga mbingu kusiwe na mvua, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo BWANA.

Kumbukumbu la Torati 28 : 24
24 BWANA atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie.

1 Wafalme 8 : 35
35 Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa;

2 Mambo ya Nyakati 7 : 13
13 Nikizifunga mbingu isiwepo mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwatumia watu wangu tauni;

Yeremia 3 : 3
3 ⑫ Kwa sababu hiyo manyunyu yamezuiliwa, wala hapakuwa na mvua ya vuli; hata hivyo ulikuwa na kipaji cha uso cha kahaba, ulikataa kutahayarika.

Amosi 4 : 7
7 Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikauka.

Zekaria 14 : 17
17 ⑪ Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, BWANA wa majeshi, mvua haitanyesha kwao.

Mwanzo 9 : 17
17 Mungu akamwambia Nuhu, Hii ndiyo ishara ya agano nililoliweka kati yangu na watu wote walioko katika nchi.

Kumbukumbu la Torati 11 : 14
14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.

Ayubu 37 : 6
6 Kwa kuwa huiambia theluji, Anguka juu ya nchi; Na pia kwa manyunyu ya mvua, Hayo manyunyu ya mvua yake nyingi.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *