Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mundu
Kumbukumbu la Torati 23 : 25
25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.
Yeremia 50 : 16
16 ⑰ Mpanzi mkatilie mbali na Babeli, Naye ashikaye mundu wakati wa mavuno; Kwa sababu ya kuuogopa upanga uoneao, Watageuka kila mtu kwa watu wake, Nao wataikimbilia kila mmoja nchi yake.
Marko 4 : 29
29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.
Yoeli 3 : 13
13 Haya! Utieni mundu, maana mavuno yameiva; njoni, kanyageni; kwa maana shinikizo limejaa, mapipa nayo yanafurika; kwani uovu wao ni mwingi sana.
Ufunuo 14 : 19
19 Malaika yule akautupa mundu wake hata nchi, akauchuma mzabibu wa nchi, akazitupa zabibu katika shinikizo hilo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
Leave a Reply