Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia mpango
Mithali 16 : 9
9 ⑬ Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake.
Yeremia 29 : 11
11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za baadaye.
Mithali 21 : 1
1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA; Kama mifereji ya maji huugeuza popote apendapo.
Yeremia 1 : 4 – 5
4 Neno la BWANA lilinijia, kusema,
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nilikujua, na kabla hujatoka tumboni, nilikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Zaburi 119 : 59
59 ⑦ Ninapozitafakari njia zako, Naielekeza miguu yangu kwa shuhuda zako.
Leave a Reply