Biblia inasema nini kuhusu mpango – Mistari yote ya Biblia kuhusu mpango

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia mpango

Mithali 16 : 9
9 ⑬ Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake.

Yeremia 29 : 11
11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za baadaye.

Mithali 21 : 1
1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA; Kama mifereji ya maji huugeuza popote apendapo.

Yeremia 1 : 4 – 5
4 Neno la BWANA lilinijia, kusema,
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nilikujua, na kabla hujatoka tumboni, nilikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

Zaburi 119 : 59
59 ⑦ Ninapozitafakari njia zako, Naielekeza miguu yangu kwa shuhuda zako.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *