Biblia inasema nini kuhusu Mlevi – Mistari yote ya Biblia kuhusu Mlevi

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mlevi

Kumbukumbu la Torati 21 : 21
21 ⑬ Wanaume wote wa mji wake na wamtupie mawe, afe; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako; na Israeli wote watasikia na kuogopa.

Zaburi 69 : 12
12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki.

Mithali 23 : 21
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.

Isaya 28 : 1
1 Ole wa taji la kiburi la walevi wa Efraimu, na ua la uzuri wa fahari yake linalonyauka, lililo kichwani mwa bonde linalositawi, la hao walioshindwa na divai!

Isaya 28 : 3
3 Taji la kiburi la walevi wa Efraimu litakanyagwa kwa miguu;

Yoeli 1 : 5
5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.

Nahumu 1 : 10
10 Kwa maana kama miiba wametatana, kama walevi wamelewa, watateketezwa kama mabua makavu.

1 Wakorintho 5 : 11
11 ⑤ Lakini, mambo yalivyo, niliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *