Biblia inasema nini kuhusu mito – Mistari yote ya Biblia kuhusu mito

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia mito

Isaya 43 : 2
2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.

Zekaria 14 : 8
8 ④ Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba maji yaliyo hai yatatoka katika Yerusalemu; nusu yake itakwenda upande wa bahari ya mashariki, na nusu yake upande wa bahari ya magharibi; wakati wa joto na wakati wa baridi itakuwa hivi.

Yohana 7 : 38
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

Mhubiri 1 : 7
7 Mito yote huingia baharini, lakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena.

Ezekieli 47 : 9
9 Tena itakuwa, kila kiumbe hai kisongamanacho, kila mahali itakapofika mito hiyo, kitaishi; kutakuwapo wingi mkubwa wa samaki, kwa sababu maji haya yamefika huko maana maji yale yatakuwa safi, na kila kitu kitaishi popote utakapofika mto huo.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *