Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia mateso
2 Wakorintho 12 : 9
9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
Zaburi 34 : 17 – 20
17 Walilia, naye BWANA akasikia, Akawaponya kutoka kwa taabu zao zote.
18 BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, Na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.
20 ⑫ Huihifadhi mifupa yake yote, Usivunjike hata mmoja.
1 Wakorintho 10 : 13
13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita muwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili muweze kustahimili.
Yakobo 5 : 11
11 Angalieni, twawaita heri wao waliostahimili. Mmesikia habari za kustahimili kwake Ayubu, kuona mwisho Bwana aliyomtendea, jinsi Bwana alivyo mwingi wa rehema na mwenye huruma.
2 Wakorintho 4 : 16
16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Warumi 8 : 18
18 Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.
Warumi 8 : 28
28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
Wafilipi 4 : 13
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Wafilipi 4 : 6
6 Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Warumi 5 : 3 – 4
3 ⑰ Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta subira;
4 na kazi ya subira ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;
Yohana 16 : 33
33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.
Zaburi 34 : 19
19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.
1 Yohana 3 : 1 – 2
1 ⑤ Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
2 ⑥ Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini tunajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.
Waraka kwa Waebrania 12 : 1
1 ⑬ Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa subira katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,
Zaburi 22 : 26
26 ⑰ Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao BWANA watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.
Zaburi 119 : 71
71 ⑮ Ilikuwa vema kwangu kuwa niliteswa, Nipate kujifunza amri zako.
Yohana 3 : 16
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Wafilipi 4 : 19
19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
Mathayo 4 : 23
23 Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya kila ugonjwa na maradhi ya kila namna waliyokuwa nayo watu.
Zaburi 34 : 1 – 22
1 Nitamhimidi BWANA kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
2 ① Katika BWANA nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie na kufurahi.
3 Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
4 ② Nilimtafuta BWANA, naye akanijibu, Akaniokoa kutoka kwa hofu zangu zote.
5 Mwelekezeeni macho, mpate kufurahi, Na nyuso zenu hazitaaibishwa kamwe.
6 ③ Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote.
7 ④ Malaika wa BWANA huwazungukia, Wamchao na kuwaokoa.
8 ⑤ Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumainia.
9 ⑥ Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake, Maana, wamchao hawapungukiwi kitu.
10 Wanasimba hutindikiwa, na kuona njaa; Bali wamtafutao BWANA hawapungukiwi kitu chochote kilicho chema.
11 Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha BWANA.
12 ⑦ Ni nani atamaniye uzima na atakaye kuishi, Siku nyingi afurahie mema?
13 ⑧ Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.
14 Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.
15 ⑩ Macho ya BWANA huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao.
16 ⑪ Uso wa BWANA ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
17 Walilia, naye BWANA akasikia, Akawaponya kutoka kwa taabu zao zote.
18 BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, Na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.
20 ⑫ Huihifadhi mifupa yake yote, Usivunjike hata mmoja.
21 ⑬ Uovu utamwua asiye haki, Nao wamchukiao mwenye haki watahukumiwa.
22 ⑭ BWANA huzikomboa nafsi za watumishi wake, Wote wamkimbiliao hawatahukumiwa.
Leave a Reply