Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia marafiki wa kweli
Mithali 18 : 24
24 Ajifanyiaye marafiki wengi ni kwa maangamizi yake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.
Yohana 15 : 13
13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
Mithali 16 : 28
28 Mtu mshupavu huleta fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.
Mithali 27 : 5 – 6
5 Lawama ya wazi ni heri, Kuliko upendo uliositirika.
6 Majeraha utiwazo na rafiki ni ya kweli; Bali busu la adui ni udanganyifu.
Mithali 27 : 17 – 27
17 Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.
18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake; Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Kama uso ufananavyo na uso katika maji; Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi; Wala macho ya wanadamu hayashibi.
21 Kalibu ni kwa fedha, na tanuri kwa dhahabu; Na mtu hujaribiwa kwa sifa zake.
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano; Upumbavu wake hautamtoka.
23 Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako; Na kuwaangalia sana ng’ombe wako.
24 Kwa maana mali haziwi za milele; Na taji je! Ladumu tangu kizazi hata kizazi?
25 Manyasi hukatwa, na majani mabichi huchipua, Na mboga ya mlimani hukusanywa.
26 Wana-kondoo hufaa kwa mavazi yako; Na mbuzi ni thamani ya shamba.
27 Tena yatakuwapo maziwa ya mbuzi, Ya kukutosha kwa chakula chako, Na chakula cha watu wa nyumbani mwako, Na posho la vijakazi vyako.
1 Yohana 4 : 1
1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zipimeni hizo roho, kama zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
Mithali 20 : 6
6 ⑤ Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe; Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?
Yohana 15 : 12 – 17
12 Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.
13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.
15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lolote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.
17 Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.
Mithali 17 : 17
17 Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.
Warumi 12 : 2
2 Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
Waraka kwa Waebrania 2 : 14
14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,
1 Wakorintho 14 : 33
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.
Leave a Reply