Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia lulu
Mathayo 13 : 45
45 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri;
Mathayo 7 : 6
6 ⑭ Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.
Mathayo 13 : 46
46 ⑧ naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua.
Mithali 31 : 10
10 Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana thamani yake yapita thamani ya marijani.
1 Timotheo 2 : 9
9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
Ayubu 28 : 18
18 Havitatajwa fedhaluka wala bilauri; Naam, kima cha hekima chapita marijani.
1 Wakorintho 6 : 19
19 ⑲ Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
Leave a Reply