Biblia inasema nini kuhusu kuwa na hukumu – Mistari yote ya Biblia kuhusu kuwa na hukumu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuwa na hukumu

Mathayo 7 : 1 – 5
1 ⑫ Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.
2 ⑬ Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.
3 Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huioni?
4 Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?
5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.

Luka 6 : 37
37 Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; sameheni, nanyi mtasamehewa.

Waefeso 2 : 9
9 ④ wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.

Mathayo 7 : 1
1 ⑫ Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.

2 Wakorintho 2 : 7
7 hata kinyume cha hayo, ni afadhali mmsamehe na kumfariji, mtu kama huyo asije akamezwa katika huzuni yake ipitayo kiasi.

Warumi 3 : 23
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

Waefeso 4 : 11 – 12
11 Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;

1 Wathesalonike 5 : 21
21 jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *