Biblia inasema nini kuhusu kuvuka mipaka – Mistari yote ya Biblia kuhusu kuvuka mipaka

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuvuka mipaka

Isaya 55 : 8 – 9
8 Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.
9 Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, ndivyo njia zangu zilivyo juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.

Isaya 40 : 22
22 Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa;

Ayubu 11 : 6 – 7
6 ⑯ Tena akuoneshe hizo siri za hekima, Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake! Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.
7 ⑰ Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu? Waweza kuufikia upeo wa huyo Mwenyezi?

Ayubu 26 : 7
7 ⑯ Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.

2 Petro 2 : 4
4 Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu;

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *