Biblia inasema nini kuhusu Kutoa – Mistari yote ya Biblia kuhusu Kutoa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kutoa

Mathayo 6 : 4
4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

1 Wakorintho 16 : 2
2 Siku ya kwanza ya juma kila mmoja wenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;

2 Wakorintho 8 : 12
12 Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.

2 Wakorintho 8 : 14
14 bali mambo yawe sawasawa; wakati huu wa sasa wingi wenu uwafae upungufu wao, ili na wingi wao uwafae ninyi mtakapopungukiwa; ili mambo yawe sawasawa.

2 Wakorintho 9 : 7
7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo mkunjufu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *