Biblia inasema nini kuhusu kusengenya – Mistari yote ya Biblia kuhusu kusengenya

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kusengenya

Waefeso 4 : 29
29 ⑮ Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.

Mithali 16 : 28
28 Mtu mshupavu huleta fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.

Mithali 6 : 16 – 19
16 Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17 ⑤ Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 ⑥ Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
19 ⑦ Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.

1 Timotheo 5 : 13
13 Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.

2 Wakorintho 12 : 20
20 Maana nachelea, nisije nikawakuta si kama vile nitakavyo kuwakuta, nikaonekana kwenu si kama vile mtakavyo; nisije nikakuta labda fitina na wivu, na ghadhabu, na ugomvi, na masingizio, na manong’onezo, na majivuno, na ghasia;

Mithali 26 : 20
20 Moto hufa kwa kukosa kuni; Na bila mchongezi fitina hukoma.

Mithali 17 : 9
9 Afunikaye kosa hutafuta kupendwa; Bali yeye afichuaye siri hutenga rafiki.

2 Timotheo 4 : 3 – 4
3 Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajikusanyia waalimu wengi, watakaowaambia yale tu masikio yao yanataka kusikia;
4 nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.

Mithali 26 : 22
22 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo. Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.

Isaya 11 : 3
3 na furaha yake itakuwa katika kumcha BWANA; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake;

Kutoka 20 : 16
16 Usimshuhudie jirani yako uongo.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *