Biblia inasema nini kuhusu kuridhika – Mistari yote ya Biblia kuhusu kuridhika

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuridhika

Yohana 6 : 35
35 Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.

Isaya 58 : 11
11 Naye BWANA atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.

Mithali 19 : 23
23 ① Kumcha BWANA huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.

Zaburi 22 : 26
26 ⑰ Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao BWANA watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.

Zaburi 145 : 16
16 Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.

Zaburi 103 : 1 – 5
1 Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA. Naam, vyote vilivyo ndani yangu Vilihimidi jina lake takatifu.
2 Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA, Wala usizisahau fadhili zake zote.
3 ⑤ Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,
4 Aukomboa uhai wako kutoka kwa kaburi, Akutia taji la fadhili na rehema,
5 Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;

Habakuki 3 : 16 – 18
16 Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.
17 Maana mtini hautachanua maua, Wala mizabibuni hamtakuwa na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, Na mashamba hayatatoa chakula; Zizini hamtakuwa na kundi, Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng’ombe;
18 Walakini nitamfurahia BWANA Nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu.

Zaburi 37 : 4
4 Nawe ujifurahishe katika BWANA, Naye atakutimizia haja za moyo wako.

Zaburi 91 : 16
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonesha wokovu wangu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *