Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuomba msaada
Yohana 14 : 13 – 14
13 ⑪ Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
14 ⑫ Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.
Zaburi 121 : 2
2 Msaada wangu hutoka kwa BWANA, Aliyezifanya mbingu na nchi.
Zaburi 121 : 1 – 8
1 Nayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?
2 Msaada wangu hutoka kwa BWANA, Aliyezifanya mbingu na nchi.
3 Hatauacha mguu wako usogezwe; Akulindaye hatasinzia;
4 Naam, hatasinzia wala hatalala, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli katika mkono wako wa kulia.
6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.
Wafilipi 4 : 13
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Leave a Reply