Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kunung’unika
Wafilipi 2 : 14
14 ① Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,
Yakobo 5 : 9
9 Ndugu, msinung’unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.
Kutoka 16 : 3
3 wana wa Israeli wakawaambia, Laiti tungalikufa kwa mkono wa BWANA katika nchi ya Misri, hapo tulipoketi karibu na zile sufuria za nyama, tulipokula vyakula hata kushiba; kwani mmetutoa huko na kututia katika bara hii, ili kutuua kwa njaa kusanyiko hili lote.
Yuda 1 : 16
16 Watu hawa ni wenye kunung’unika, wenye kulalamika, waendao kwa tamaa zao, na vinywa vyao vyanena maneno makuu mno ya kiburi, wakipendelea watu wenye cheo kwa ajili ya faida.
Kutoka 15 : 24
24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?
1 Wakorintho 10 : 10
10 Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakauawa na mharibifu.
Leave a Reply