Biblia inasema nini kuhusu Kumngoja Mungu – Mistari yote ya Biblia kuhusu Kumngoja Mungu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kumngoja Mungu

Yeremia 14 : 22
22 ② Je! Katika vitu vya ubatili vya mataifa, kiko kitu kiwezacho kuleta mvua? Je! Mbingu zaweza kutoa manyunyu? Je! Si wewe, Ee BWANA, Mungu wetu? Kwa sababu hiyo tutakungoja; kwa kuwa wewe umevifanya vitu hivi vyote.

Zaburi 25 : 5
5 Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.

Zaburi 104 : 28
28 Wewe huwapa, Wao wanakiokota; Wewe waukunjua mkono wako, Wao wanashiba mema;

Zaburi 145 : 16
16 Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.

Zaburi 123 : 2
2 Kama vile macho ya watumishi Yanavyoutegemea mkono wa bwana zao Kama macho ya mjakazi Yanavyoutegemea mkono wa bimkubwa wake; Ndivyo macho yetu yanavyomtegemea BWANA, Mungu wetu, Hadi atakapoturehemu.

Zaburi 39 : 8
8 Uniokoe kutoka kwa maasi yangu yote, Usinifanye niwe wa kulaumiwa na mpumbavu.

Luka 2 : 25
25 Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.

Mwanzo 49 : 18
18 Wokovu wako nimeungoja, Ee BWANA.

Zaburi 62 : 2
2 Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika.

Zaburi 25 : 5
5 Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.

Zaburi 33 : 20
20 Nafsi zetu zinamngoja BWANA; Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.

Zaburi 59 : 10
10 Mungu wa fadhili zangu atanitangulia, Mungu atanijalia kutazama kwa ushindi juu ya adui zangu.

Habakuki 2 : 3
3 Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.

Matendo 1 : 4
4 Wakati alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kutoka kwangu;

Wagalatia 5 : 5
5 Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

1 Wakorintho 1 : 7
7 hata hamkupungukiwa na karama yoyote, mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo;

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *