Biblia inasema nini kuhusu kukopa – Mistari yote ya Biblia kuhusu kukopa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kukopa

Zaburi 37 : 21
21 Asiye haki hukopa wala halipi, Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu.

Mithali 22 : 7
7 Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.

Mathayo 5 : 42
42 Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.

Mithali 22 : 26 – 27
26 Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu;
27 Kama huna kitu cha kulipa; Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *