Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kukopa
Zaburi 37 : 21
21 Asiye haki hukopa wala halipi, Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu.
Mithali 22 : 7
7 Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.
Mathayo 5 : 42
42 Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
Mithali 22 : 26 – 27
26 Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu;
27 Kama huna kitu cha kulipa; Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?
Leave a Reply