Biblia inasema nini kuhusu Kukata tamaa โ€“ Mistari yote ya Biblia kuhusu Kukata tamaa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kukata tamaa

Hesabu 17 : 13
13 Kila mtu akaribiaye, aikaribiaye maskani ya BWANA, hufa; je! Tutakufa sote pia?

Kumbukumbu la Torati 28 : 67
67 โ‘ฏ asubuhi utasema, Laiti ingekuwa jioni! Na jioni utasema, Laiti ingekuwa asubuhi! Kwa kicho cha moyo wako utakavyokucha, na kuona kwa macho yako utakavyoona.

Ayubu 3 : 26
26 Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini taabu huja.

Ayubu 17 : 16
16 Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu, Itakapokuwapo raha mavumbini.

Zaburi 31 : 22
22 Nami nilisema kwa pupa yangu, Nimekatiliwa mbali na macho yako; Lakini ulisikia sauti ya kilio changu Wakati nilipokulilia.

Zaburi 77 : 9
9 โ‘ฐ Mungu amesahau fadhili zake? Amezuia kwa hasira rehema zake?

Mithali 13 : 12
12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.

Isaya 2 : 19
19 โ‘  Na watu wataingia ndani ya pango za majabali, na ndani ya mashimo ya nchi, mbele za utisho wa BWANA na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili aitetemeshe mno dunia.

Yeremia 2 : 25
25 Zuia mguu wako usikose kiatu, na koo yako isiwe na kiu; lakini wewe ulisema, Hakuna matumaini kabisa; la, maana nimewapenda wageni, nami nitawafuata.

Yeremia 8 : 20
20 Mavuno yamepita, wakati wa joto umekwisha, wala sisi hatukuokoka.

Yeremia 18 : 12
12 Lakini wao wasema, Hakuna tumaini lolote; maana sisi tutafuata mawazo yetu wenyewe, nasi tutatenda kila mmoja wetu kwa kuufuata ushupavu wa moyo wake mbaya.

Maombolezo 3 : 21
21 Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini.

Maombolezo 5 : 22
22 Ingawa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.

Hosea 10 : 8
8 Mahali pa Aveni palipoinuka, yaani, dhambi ya Israeli, pataharibika; mwiba na mbigili itamea juu ya madhabahu zake; nao wataiambia milima, Tusitirini; na vilima, Tuangukieni.

Yona 2 : 4
4 Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako; Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu.

Mika 7 : 7
7 Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.

Mathayo 24 : 30
30 โ‘  ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi.

Luka 13 : 28
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.

Luka 23 : 30
30 Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.

Ufunuo 6 : 17
17 โ‘ฑ Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kuistahimili?

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *