Biblia inasema nini kuhusu kujua yote – Mistari yote ya Biblia kuhusu kujua yote

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kujua yote

Zaburi 147 : 5
5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

1 Yohana 3 : 20
20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.

Yeremia 1 : 5
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nilikujua, na kabla hujatoka tumboni, nilikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

Isaya 40 : 28
28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.

Yeremia 23 : 24
24 ⑩ Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone? Asema BWANA. Je! Mbingu na nchi hazikujawa nami? Asema BWANA.

Zaburi 147 : 4 – 5
4 Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.
5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

Zaburi 139 : 1 – 6
1 ⑰ Ee BWANA, umenichunguza na kunijua.
2 ⑱ Wewe wajua kuketi kwangu na kusimama kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali.
3 Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.
4 ⑲ Maana hamna neno katika ulimini wangu Usilolijua kabisa, BWANA.
5 Umenizingira nyuma na mbele, Ukaniwekea mkono wako.
6 Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.

Isaya 40 : 13 – 14
13 Ni nani aliyemwongoza Roho ya BWANA, na kumfundisha kwa kuwa mshauri wake?
14 Alifanya shauri na nani, ni nani aliyemwelimisha na kumfunza njia ya hukumu, na kumfunza maarifa, na kumwonesha njia ya fahamu?

Mathayo 10 : 30
30 lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.

1 Wakorintho 2 : 11
11 Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

Matendo 1 : 24
24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuoneshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

Warumi 11 : 33 – 36
33 ⑳ Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazieleweki!
34 Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake?
35 Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena?
36 Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.

1 Mambo ya Nyakati 28 : 9
9 ⑦ Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele.

Waraka kwa Waebrania 4 : 13
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, maana vitu vyote ni tupu na kuwekwa wazi machoni pake yeye ambaye tunapaswa kuwajibika kwake.

Yeremia 29 : 11
11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za baadaye.

Kumbukumbu la Torati 29 : 29
29 Mambo ya siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii.

Warumi 8 : 29
29 Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *