Biblia inasema nini kuhusu kuaga – Mistari yote ya Biblia kuhusu kuaga

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuaga

Hesabu 6 : 24 – 26
24 ⑪ BWANA akubariki, na kukulinda;
25 ⑫ BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
26 ⑬ BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.

Mhubiri 3 : 1 – 15
1 ④ Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 ⑤ Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa kilichopandwa;
3 ⑥ Wakati wa kuua, na wakati wa kuponya; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 ⑦ Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 ⑧ Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 ⑩ Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.
9 ⑪ Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?
10 ⑫ Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
11 ⑬ Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.
12 Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.
13 ⑭ Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
14 ⑮ Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye.
15 ⑯ Yale yaliyoko yamekuwako; na hayo yatakayokuwako yamekwisha kuwako; naye Mungu huyatafuta tena mambo yale yaliyopita.

Zaburi 21 : 6
6 Maana umemfanya kuwa baraka za milele, Wamfurahisha kwa furaha ya uso wako.

Waefeso 6 : 10
10 ⑥ Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

Zaburi 121 : 1 – 8
1 Nayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?
2 Msaada wangu hutoka kwa BWANA, Aliyezifanya mbingu na nchi.
3 Hatauacha mguu wako usogezwe; Akulindaye hatasinzia;
4 Naam, hatasinzia wala hatalala, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli katika mkono wako wa kulia.
6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Mwanzo 24 : 56
56 ③ Naye akawaambia, Msinikawilishe, mradi BWANA amefanikisha njia yangu; nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *