Biblia inasema nini kuhusu Kor – Mistari yote ya Biblia kuhusu Kor

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kor

Ezekieli 45 : 14
14 na sehemu ya mafuta iliyoamriwa, katika bathi ya mafuta, itakuwa sehemu ya kumi ya bathi katika kori moja, ambayo ni bathi kumi, yaani homeri; maana bathi kumi ni homeri moja;

1 Wafalme 4 : 22
22 Na vyakula vya Sulemani vya siku moja vilikuwa kori[2] thelathini za unga mzuri, na kori sitini za ngano,

1 Wafalme 5 : 11
11 Sulemani akampa Hiramu kori[4] elfu ishirini za ngano, chakula cha watu wake, na kori ishirini za mafuta safi. Ndizo Sulemani alizompa Hiramu mwaka kwa mwaka.

2 Mambo ya Nyakati 2 : 10
10 Na tazama, nitawapa watumishi wako, wachongaji wakatao miti, kori[3] elfu ishirini za ngano iliyopondwa, na kori elfu ishirini za shayiri, na bathi elfu ishirini za mvinyo na bathi[4] elfu ishirini za mafuta.

2 Mambo ya Nyakati 27 : 5
5 ⑰ Kisha akapigana na mfalme wa Waamoni, akawashinda. Na Waamoni wakampa mwaka ule ule talanta mia moja za fedha, na kori elfu kumi za ngano, na elfu kumi za shayiri. Hayo ndiyo waliyomtolea Waamoni, mwaka wa pili pia, na mwaka wa tatu.

Ezra 7 : 22
22 hata kiasi cha talanta mia moja za fedha, na vipimo mia vya ngano, na bathi mia moja za divai, na bathi mia moja za mafuta na chumvi ya kiasi chochote kile.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *