Biblia inasema nini kuhusu kivuli – Mistari yote ya Biblia kuhusu kivuli

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kivuli

Zaburi 57 : 1
1 Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi, Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe. Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako, Hadi misiba hii itakapopita.

Yakobo 1 : 17
17 Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.

Wakolosai 2 : 16 – 17
16 ⑱ Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
17 ⑲ mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *