Biblia inasema nini kuhusu Kitimu – Mistari yote ya Biblia kuhusu Kitimu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kitimu

Mwanzo 10 : 4
4 Na wana wa Yavani ni Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Warodani.

Isaya 23 : 1
1 Ufunuo juu ya Tiro. Toeni sauti za uchungu, enyi merikebu za Tarshishi, kwa maana umeharibika kabisa, hata hapana nyumba, hapana mahali pa kuingia; toka nchi ya Kitimu wamefunuliwa habari.

Isaya 23 : 12
12 Naye akasema, Usizidi kufurahi, ewe bikira uliyeaibishwa, binti wa Sidoni, haya, ondoka, uende hadi Kitimu; huko nako hutapata raha.

Yeremia 2 : 10
10 Maana, vukeni mpaka visiwa vya Kitimu, mkaone; tumeni watu waende Kedari, mkafikiri sana; mkaone kwamba jambo kama hili limekuwa wakati wowote.

Ezekieli 27 : 6
6 kwa mialoni ya Bashani wamefanya makasia yako; na sitaha zako wamezifanya kwa pembe iliyotiwa kazi ya njumu katika mti wa mihugu itokayo Kitimu.

Hesabu 24 : 24
24 Lakini merikebu zitakuja kutoka pwani kwa Kitimu, Nazo zitamtaabisha Ashuru, na Eberi zitamtaabisha, Yeye naye atapata uharibifu.

Danieli 11 : 30
30 Maana merikebu za Kitimu zitakuja kupigana naye; basi atavunjika moyo, naye atarudi na kulighadhibikia hilo agano takatifu; na kutenda kadiri apendavyo; naam, atarudi, na kuwasikiliza walioacha hilo agano takatifu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *