Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kashfa
Luka 6 : 45
45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.
Zaburi 109 : 3
3 Naam, kwa maneno ya chuki wamenizunguka, Wamepigana nami bure.
1 Timotheo 5 : 13
13 Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.
Zaburi 50 : 20
20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.
Mithali 11 : 9
9 Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake; Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
Ufunuo 12 : 10
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
Zaburi 52 : 4
4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.
Mithali 10 : 18
18 Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.
Tito 2 : 3
3 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wanaofundisha yaliyo mema;
1 Timotheo 3 : 11
11 ⑧ Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; wasiwe wachongezi; ila wawe watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
Zaburi 35 : 11
11 Mashahidi wa udhalimu wanasimama, Wananiuliza mambo nisiyoyajua.
Mathayo 26 : 60
60 wasiuone ingawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.
Warumi 3 : 8
8 Kwa nini tusiseme (kama tulivyosingiziwa, na kama wengine wanavyokaza kusema ya kwamba twasema hivyo), Na tufanye mabaya, ili yaje mema? Ambao kuhukumiwa kwao kuna haki.
2 Wakorintho 6 : 8
8 kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli;
Zaburi 50 : 20
20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.
Leave a Reply