Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Jahazi
Yoshua 13 : 18
18 na Yahasa, na Kedemothi, na Mefaathi;
Yoshua 21 : 36
36 Tena katika kabila la Reubeni, Bezeri pamoja na mbuga zake za malisho, na Yahasa pamoja na mbuga zake za malisho,
Isaya 15 : 4
4 Heshboni analia na Eleale; mpaka Yahasa sauti ya kulia kwao inasikiwa; hata watu wa Moabu waliovaa silaha wanapiga kelele sana kwa sababu hiyo; nafsi yake inatetemeka ndani yake.
Yeremia 48 : 21
21 Na hukumu imeifikia nchi tambarare; juu ya Holoni, na juu ya Yasa, na juu ya Mefaathi;
Hesabu 21 : 23
23 ⑥ Lakini Sihoni hakukubali kumwacha Israeli kupita katika mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, akatoka aende kupigana na Israeli jangwani, akafika mpaka Yahasa; akapigana na Israeli.
Kumbukumbu la Torati 2 : 32
32 Ndipo Sihoni alipojitokeza juu yetu, yeye na watu wake wote ili kupigana nasi huko Yahasa.
Waamuzi 11 : 20
20 Lakini huyo Sihoni hakuwaamini Israeli ili wapite ndani ya mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, nao wakapiga kambi katika Yahasa, wakapigana na Israeli.
Leave a Reply