Biblia inasema nini kuhusu Ikulu – Mistari yote ya Biblia kuhusu Ikulu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Ikulu

1 Wafalme 21 : 1
1 Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria.

2 Wafalme 15 : 25
25 Na Peka mwana wa Remalia, jemadari wake, akamfanyia uhaini, akampiga huko Samaria, katika ngome ya nyumba ya mfalme, pamoja na Argobu na Arie; na pamoja naye walikuwako watu hamsini wa Wagileadi. Akamwua, akatawala mahali pake.

Yeremia 49 : 27
27 Nami nitawasha moto katika ukuta wa Dameski, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi.

Amosi 1 : 12
12 lakini nitatuma moto juu ya Temani, nao utayateketeza majumba ya Bosra.

Nahumu 2 : 6
6 Malango ya mito yamefunguka, na jumba la mfalme limeyeyushwa.

2 Samweli 7 : 2
2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.

1 Wafalme 7 : 12
12 ③ Na behewa kubwa pande zote ilikuwa na safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi; mfano wa behewa ya ndani ya nyumba ya BWANA, na ukumbi wa nyumba.

Danieli 4 : 29
29 Baada ya miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli.

Danieli 5 : 5
5 ⑧ Saa iyo hiyo vikatokea vidole vya mkono wa mwanadamu, vikaandika katika chokaa ya ukuta wa nyumba ya enzi ya mfalme, mahali palipokielekea kinara; naye mfalme akakiona kiganja cha ule mkono ulioandika.

Danieli 6 : 18
18 Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa.

Nehemia 1 : 1
1 Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kislevu,[1] mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni,

Esta 1 : 2
2 siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Susa, mji mkuu ngomeni;

Esta 7 : 7
7 Mfalme akaondoka kwa ghadhabu kutoka kwenye karamu ya divai, akaingia bustani ya ngome. Hamani naye akasimama ili ajitakie maisha yake kwa malkia Esta; kwa kuwa aliona ya kwamba amekusudiwa madhara na mfalme.

Danieli 8 : 2
2 Nami niliona katika maono; nilipokuwa natazama na nikajionea mwenyewe nikiwa huko Susa, Mji mkuu wa mkoa wa Elamu; nikaona katika maono, nami nilikuwa karibu na mto Ulai.

Ezra 6 : 2
2 Na kitabu kimoja kilipatikana huko Akmetha, katika nyumba ya mfalme iliyo katika wilaya ya Umedi, na ndani yake maneno haya yameandikwa ili yakumbukwe.

Amosi 3 : 9
9 Tangazeni habari katika majumba ya Ashdodi, na katika majumba ya nchi ya Misri, mkaseme, Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria, katazameni, ni mishindo mikubwa kama nini iliyomo humo, na udhalimu mwingi kama nini uliomo ndani yake.

Amosi 1 : 12
12 lakini nitatuma moto juu ya Temani, nao utayateketeza majumba ya Bosra.

Amosi 2 : 2
2 lakini nitatuma moto juu ya Moabu, nao utayateketeza majumba ya Keriothi; na Moabu atakufa pamoja na mshindo, na kelele, na sauti ya tarumbeta;

Nahumu 2 : 6
6 Malango ya mito yamefunguka, na jumba la mfalme limeyeyushwa.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *