Biblia inasema nini kuhusu ibada – Mistari yote ya Biblia kuhusu ibada

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia ibada

Zaburi 95 : 6
6 ③ Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.

Yohana 4 : 24
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Wakolosai 3 : 14 – 17
14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.
15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kupitia kwake.

Warumi 12 : 1
1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

Isaya 12 : 5
5 Mwimbieni BWANA; kwa kuwa ametenda makuu; Na yajulikane haya katika dunia yote.

Waraka kwa Waebrania 13 : 15
15 ⑤ Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamalo jina lake.

Yohana 4 : 23
23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Waraka kwa Waebrania 12 : 28
28 Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na muwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;

Mathayo 18 : 20
20 ⑩ Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.

Luka 4 : 8
8 ⑳ Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.

Zaburi 132 : 7
7 Na tuingie katika maskani yake, Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake.

Zaburi 95 : 1 – 6
1 Njoni, tumwimbie BWANA, Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
2 Tuje mbele zake kwa shukrani, Tumfanyie shangwe kwa zaburi.
3 Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu, Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia, Hata vilele vya milima ni vyake.
5 Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya, Na mikono yake iliumba nchi kavu.
6 ③ Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.

Zaburi 29 : 2
2 Mpeni BWANA utukufu wa jina lake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu.

Isaya 56 : 7
7 Nitawaleta hao nao hadi katika mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.

Ufunuo 14 : 7
7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.

Ufunuo 19 : 10
10 ⑳ Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.

1 Petro 2 : 5
5 ③ Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa muwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

Zaburi 99 : 5
5 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu; Sujuduni penye kiti cha miguu yake; Ndiye mtakatifu.

Waraka kwa Waebrania 10 : 25
25 ⑫ wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri muonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Zaburi 77 : 13
13 ⑳ Ee Mungu, njia yako iko katika utakatifu; Ni Mungu yupi aliye mkuu kama Mungu wetu?

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *