Biblia inasema nini kuhusu hasira – Mistari yote ya Biblia kuhusu hasira

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia hasira

Waefeso 4 : 31
31 ⑰ Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matusi yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;

Waefeso 4 : 31 – 32
31 ⑰ Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matusi yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;
32 ⑱ tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Yakobo 1 : 19 – 20
19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
20 kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.

Mithali 16 : 32
32 Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.

Mithali 15 : 1
1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Mithali 29 : 11
11 Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

Wakolosai 3 : 8
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na masuto, na matusi vinywani mwenu.

Mithali 14 : 17
17 Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.

Waefeso 4 : 26 – 27
26 ⑬ Muwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;
27 wala msimpe Ibilisi nafasi.

Waefeso 4 : 32
32 ⑱ tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Warumi 12 : 21
21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

Mithali 15 : 1 – 33
1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
2 Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
3 Macho ya BWANA yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.
4 Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5 Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
6 Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
7 Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
8 Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
9 Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
10 Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11 Kuzimu na Uharibifu viko wazi mbele za BWANA; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12 Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13 Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa; Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15 Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya; Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16 ① Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17 Chakula cha mboga palipo na upendo; Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
18 Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
19 Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21 ② Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22 Pasipo ushauri mipango vuhunjika; Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.
23 Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24 ③ Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.
25 BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26 Ushauri mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maneno yapendezayo ni safi.
27 ④ Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.
28 ⑤ Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
29 ⑥ BWANA yuko mbali na wasio haki; Bali huisikia sala ya mwenye haki.
30 Mng’ao wa macho huufurahisha moyo; Habari njema huinenepesha mifupa.
31 Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.
32 Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.
33 Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *