Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Haki
Mwanzo 15 : 6
6 Akamwamini BWANA, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
Warumi 4 : 3
3 Maana Maandiko yasemaje? Abrahamu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa haki.
Warumi 4 : 5
5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki.
Warumi 4 : 9
9 Basi je! Heri hiyo ni kwa hao waliotahiriwa, au kwa hao pia wasiotahiriwa? Kwa kuwa tunanena ya kwamba kwake Abrahamu imani yake ilihesabiwa kuwa ni haki.
Warumi 4 : 11
11 Naye aliipokea dalili hii ya kutahiriwa, mhuri wa ile haki ya imani aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa; apate kuwa baba yao wote waaminio, ijapokuwa hawakutahiriwa, ili na wao pia wahesabiwe haki;
Warumi 4 : 13
13 ② Kwa maana ahadi ile ya kwamba atakuwa mrithi wa ulimwengu alipewa Abrahamu na uzao wake, si kwa sheria bali kwa haki aliyohesabiwa kwa imani.
Warumi 4 : 20
20 ⑩ Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutoamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;
Warumi 4 : 22
22 ⑪ Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.
Warumi 4 : 24
24 ⑬ bali na kwa ajili yetu sisi mtakaohesabiwa vivyo hivyo, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu katika wafu;
Ayubu 29 : 14
14 ① Nilijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba.
Mathayo 22 : 14
14 Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.
Kumbukumbu la Torati 6 : 25
25 Tena itakuwa haki kwetu, tukizingatia kufanya maagizo haya yote mbele ya BWANA, Mungu wetu, kama alivyotuagiza.
Ayubu 33 : 26
26 ⑥ Yeye humwomba Mungu, naye akamtakabalia; Hata auone uso wake kwa furaha; Naye humrejeshea mtu haki yake.
Kumbukumbu la Torati 6 : 25
25 Tena itakuwa haki kwetu, tukizingatia kufanya maagizo haya yote mbele ya BWANA, Mungu wetu, kama alivyotuagiza.
Yoshua 22 : 31
31 Naye Finehasi, mwana wa Eleazari, kuhani, akawaambia wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na wana wa Manase, akasema, Siku hii ya leo tumejua ya kwamba BWANA yu kati yetu, kwa sababu hamkukosa katika jambo hili mbele ya BWANA; sasa ninyi mmewaokoa wana wa Israeli na mkono wa BWANA.
Zaburi 1 : 3
3 Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
Zaburi 15 : 5
5 Asiyetoa fedha yake apate kula riba, Asiyepokea rushwa amwangamize asiye na hatia. Mtu atendaye mambo hayo Hataondoshwa milele.
Zaburi 24 : 5
5 Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.
Zaburi 101 : 4
4 Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu, Lililo ovu sitalijua.
Zaburi 106 : 3
3 Heri washikao hukumu, Na kutenda haki sikuzote.
Zaburi 112 : 8
8 Moyo wake umethibitika hataogopa, Hata awaone watesi wake wameshindwa.
Mithali 2 : 20
20 Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, Na kuyashika mapito ya wenye haki.
Mithali 10 : 2
2 ⑦ Hazina za uovu hazifaidii kitu; Bali haki huokoa na mauti.
Mithali 11 : 6
6 Haki yao wenye haki itawaokoa; Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.
Mithali 11 : 19
19 Haki huelekea uzima; Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.
Mithali 11 : 30
30 Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima; Na mwenye hekima huvuta roho za watu.
Leave a Reply