Biblia inasema nini kuhusu furaha – Mistari yote ya Biblia kuhusu furaha

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia furaha

Zaburi 37 : 4
4 Nawe ujifurahishe katika BWANA, Naye atakutimizia haja za moyo wako.

Mhubiri 3 : 12
12 Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.

Wafilipi 4 : 4
4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

Isaya 12 : 2
2 Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu.

Wafilipi 4 : 7
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Mithali 3 : 13 – 18
13 Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.
14 ⑪ Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 ⑫ Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.
16 ⑬ Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kulia, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.
17 ⑭ Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.
18 ⑮ Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu anayeshikamana naye.

Mithali 14 : 13
13 Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni; Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.

Mhubiri 3 : 13
13 ⑭ Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.

Isaya 12 : 3
3 Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu.

1 Petro 3 : 14
14 Lakini hata mkiteswa kwa sababu ya kutenda haki, mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.

Zaburi 37 : 3
3 Umtumaini BWANA ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.

1 Petro 4 : 12
12 ④ Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

Ayubu 5 : 17 – 27
17 ⑪ Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.
18 ⑫ Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza; Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.
19 ⑬ Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.
20 Wakati wa njaa atakukomboa na mauti; Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.
21 ⑭ Utafichwa na mapigo ya ulimi; Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.
22 Wewe utayacheka maangamizo na njaa; Wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi.
23 ⑮ Kwani utakuwa na mapatano na mawe ya bara; Nao wanyama wa bara watakuwa na amani kwako.
24 Nawe utajua ya kwamba hema yako ni salama; Na zizi lako utalikagua, wala usikose kitu.
25 Tena utajua ya kwamba uzao wako utakuwa mwingi, Na uzao wako utakuwa kama nyasi za nchi.
26 Utafika kaburini mwenye umri mtimilifu, Kama mganda wa ngano ulivyo wakati wake.
27 Tazama, haya tumeyapeleleza, ndivyo yalivyo; Yasikie, uyajue, ili upate mema.

2 Wakorintho 12 : 10
10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na matusi, na matatizo, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

Warumi 5 : 2
2 ⑯ ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu.

Zaburi 40 : 8
8 ⑱ Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.

Mhubiri 3 : 22
22 Hivyo nikaona ya kwamba hakuna jema kupita mwanadamu kuzifurahia kazi zake; kwa sababu hili ni fungu lake; kwa maana ni nani atakayemrudisha tena ili ayaone yatakayomfuata baadaye.

Mithali 14 : 21
21 Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.

Waraka kwa Waebrania 11 : 1
1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni kusadiki mambo yasiyoonekana.

Luka 16 : 25
25 Abrahamu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo yako mema katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unateseka.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *