Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Falsafa
Ayubu 5 : 20
20 Wakati wa njaa atakukomboa na mauti; Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.
Ayubu 10 : 21
21 ⑭ Kabla sijaenda huko ambako sitarudi kutoka huko tena, Ni hiyo nchi ya giza, giza tupu;
Ayubu 12 : 24
24 Huwaondolea moyo wakuu wa watu wa nchi, Na kuwapoteza nyikani pasipokuwa na njia.
Ayubu 33 : 30
30 ⑦ Ili kurudisha roho yake itoke shimoni, Ili atiwe mwanga kwa mwanga wa walio hai.
Mithali 25 : 2
2 ⑪ Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.
Warumi 1 : 20
20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru;
1 Wakorintho 1 : 22
22 Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
1 Wakorintho 2 : 10
10 ⑤ Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.
1 Wakorintho 1 : 17
17 Maana Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika.
1 Wakorintho 1 : 19
19 Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
1 Wakorintho 1 : 21
21 Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.
1 Wakorintho 2 : 5
5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.
1 Wakorintho 2 : 13
13 ⑦ Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni.
Leave a Reply