Biblia inasema nini kuhusu Ekaristi – Mistari yote ya Biblia kuhusu Ekaristi

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Ekaristi

Mathayo 26 : 30
30 ⑥ Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda katika mlima wa Mizeituni.

Marko 14 : 24
24 ③ Akawaambia, Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.

Luka 22 : 20
20 ⑬ Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]

Yohana 13 : 4
4 aliondoka chakulani; akaweka kando mavazi yake, akatwaa kitambaa, akajifunga kiunoni.

Luka 13 : 26
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

Matendo 2 : 42
42 ⑳ Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

Matendo 2 : 47
47 wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.

Matendo 20 : 7
7 ⑪ Siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubia, maana aliazimia kusafiri siku iliyofuata, naye akafululiza maneno yake hadi usiku wa manane.

1 Wakorintho 10 : 17
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

1 Wakorintho 10 : 22
22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?

1 Wakorintho 11 : 34
34 mtu akiwa na njaa, na ale nyumbani kwake; msipate kukutanika kwa hukumu. Na hayo yaliyosalia nikija nitayatengeneza.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *