Biblia inasema nini kuhusu Deni – Mistari yote ya Biblia kuhusu Deni

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Deni

Warumi 13 : 8
8 ③ Msiwiwe na mtu chochote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.

Kutoka 22 : 27
27 maana hiyo nguo ni kifuniko chake, hiyo peke yake ni nguo ya ngozi yake; je! Atalalia nini? Itakuwa, hapo atakaponililia mimi, nitasikia; kwa kuwa mimi ni mwenye rehema.

Kumbukumbu la Torati 24 : 6
6 ⑤ Mtu awaye yote asitwae jiwe la kusagia, la juu wala la chini, kuwa rehani; kwani hivi ni kutwaa maisha ya mtu kuwa rehani.

Kumbukumbu la Torati 24 : 13
13 ⑪ Sharti umrudishie rehani lichwapo jua, apate kulala na mavazi yake, na kukubarikia; nayo itakuwa ni haki kwako mbele za BWANA, Mungu wako.

Nehemia 5 : 4
4 Tena walikuwako wengine waliosema, Tumekopa fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa kuweka rehani mashamba yetu, na mizabibu yetu.

Ayubu 22 : 6
6 Kwa kuwa umetwaa dhamana kwa nduguyo bure, Na kuwavua nguo zao walio uchi.

Ayubu 24 : 9
9 Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba, Na kutwaa rehani kwa maskini;

Mithali 11 : 15
15 Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yuko salama.

Mithali 22 : 26
26 Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu;

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *