Biblia inasema nini kuhusu dawa – Mistari yote ya Biblia kuhusu dawa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia dawa

Ezekieli 47 : 12
12 Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayataisha kamwe; utatoa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu maji yake yanatoka mahali patakatifu; na matunda yake yatakuwa ni chakula; na majani yake yatakuwa ni dawa.

1 Timotheo 5 : 23
23 Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara.

Isaya 38 : 21
21 Maana Isaya amesema, Na watwae mkate wa tini, wakauweke juu ya jipu, naye atapona.

Luka 10 : 34
34 akakaribia, akamfunga majeraha yake, akayatia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

Mithali 17 : 22
22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri; Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.

Mathayo 9 : 12
12 Naye aliposikia, aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.

Yeremia 8 : 22
22 ③ Je! Hakuna marhamu katika Gileadi? Huko hakuna tabibu? Mbona, basi, haijarejea afya ya binti ya watu wangu?

Yakobo 5 : 15
15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.

Zaburi 103 : 3
3 ⑤ Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,

Ufunuo 22 : 2
2 katikati ya njia yake kuu. Na upande huu na huu kando ya ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.

Yeremia 46 : 11
11 ⑯ Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe.

Yeremia 30 : 13
13 Hapana mtu wa kukutetea; kwa jeraha lako huna dawa ziponyazo.

Ayubu 5 : 18
18 ⑫ Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza; Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.

Warumi 12 : 2
2 Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Marko 5 : 24 – 29
24 Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsongasonga.
25 Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,
26 na kuvumilia mateso mengi kutoka kwa matabibu wengi, na kugharimiwa mali yake yote aliyokuwa nayo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27 Aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake;
28 maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona.
29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule.

Mhubiri 3 : 3
3 ⑥ Wakati wa kuua, na wakati wa kuponya; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

Zaburi 147 : 3
3 Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuyaganga majeraha yao.

Mwanzo 50 : 2
2 ⑧ Yusufu akawaagiza watumishi wake waganga wampake baba yake dawa asioze. Waganga wakampaka dawa Israeli.

Isaya 1 : 6
6 Toka wayo wa mguu hadi kichwani hamna uzima ndani yake; bali jeraha na machubuko na vidonda vitokavyo usaha; havikufungwa, havikuzongwazongwa, wala havikulainishwa kwa mafuta.

Ezekieli 34 : 4
4 Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *