Biblia inasema nini kuhusu Busara – Mistari yote ya Biblia kuhusu Busara

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Busara

Ayubu 34 : 4
4 Na tujichagulie yaliyo ya uelekevu; Na tujue wenyewe yaliyo mema.

Zaburi 39 : 1
1 ⑧ Nilisema, Nitazitunza njia zangu Nisije nikakosa kwa ulimi wangu; Nitajitia lijamu kinywani, Maadamu mtu mbaya awapo mbele yangu.

Zaburi 112 : 5
5 ⑱ Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.

Mithali 6 : 2
2 Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,

Mithali 8 : 12
12 Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa makao yangu; Natafuta maarifa na busara.

Mithali 11 : 13
13 Mwenye udaku hupitapita akifunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

Mithali 11 : 15
15 Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yuko salama.

Mithali 11 : 29
29 Ataabishaye nyumba yake mwenyewe ataurithi upepo; Mpumbavu atakuwa mtumwa wa mtu mwenye moyo wa akili.

Mithali 12 : 8
8 Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake; Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.

Mithali 12 : 16
16 Ghadhabu ya mpumbavu hujulikana mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.

Mithali 12 : 23
23 Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.

Mithali 13 : 16
16 ⑰ Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa; Bali mpumbavu hueneza upumbavu.

Mithali 14 : 8
8 Akili za mwenye busara ni kujua njia yake; Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

Mithali 14 : 16
16 Mwenye hekima huhadhari, na kujitenga na uovu; Bali mpumbavu hupuuza yote, na hajali.

Mithali 14 : 18
18 Wajinga hurithi upumbavu; Bali wenye busara huvikwa taji la maarifa.

Mithali 15 : 5
5 Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.

Mithali 15 : 22
22 Pasipo ushauri mipango vuhunjika; Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.

Mithali 16 : 21
21 Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara; Utamu wa maneno huongeza elimu.

Mithali 17 : 2
2 Mtumwa atendaye kwa busara atamtawala mwana atendaye mambo ya aibu; Tena atapata sehemu ya urithi kati ya ndugu.

Mithali 17 : 18
18 Asiye na hekima hupeana mkono na mtu; Na kuwa mdhamini wa mtu mwingine.

Mithali 18 : 16
16 Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu.

Mithali 19 : 2
2 Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

Mithali 20 : 5
5 Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.

Mithali 20 : 16
16 Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni; Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.

Mithali 20 : 18
18 Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.

Mithali 21 : 5
5 Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

Mithali 21 : 20
20 Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *