Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Anga
Mwanzo 1 : 8
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
Mwanzo 1 : 17
17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi
Mwanzo 1 : 20
20 Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na viumbe vyenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.
Zaburi 19 : 1
1 Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.
Danieli 12 : 3
3 Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota milele na milele.
Leave a Reply