Biblia inasema nini kuhusu Amoni โ€“ Mistari yote ya Biblia kuhusu Amoni

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Amoni

1 Wafalme 22 : 26
26 Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya, mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme;

2 Mambo ya Nyakati 18 : 25
25 Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji, na kwa Yoashi mwana wa mfalme;

2 Wafalme 21 : 26
26 Akazikwa kaburini mwake katika bustani ya Uza. Na Yosia mwanawe akatawala mahali pake.

2 Mambo ya Nyakati 33 : 25
25 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliomfanyia fitina mfalme Amoni; watu wa nchi wakamfanya Yosia mwanawe awe mfalme badala yake.

Sefania 1 : 1
1 Neno la BWANA lililomjia Sefania, mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia; katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda.

Mathayo 1 : 10
10 Hezekia akamzaa Manase; Manase akamzaa Amoni; Amoni akamzaa Yosia;

Nehemia 7 : 59
59 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-Sebaimu, wana wa Amoni.

Ezra 2 : 57
57 wazawa wa Shefatia, wazawa wa Hatili, wazawa wa Pokereth-Sebaimu, wazawa wa Amoni.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *